Friday, December 28, 2012

0

SABABU ZA P UNIT KUWA PAMOJA MPAKA LEO


 

Baada Ya kipindi kirefu cha kufanya kazi pamoja kama Kundi, wasanii wanaounda P Unit, Frasha, Gabu pamoja na Bon-Eye wameweka hadharani siri yao ya kuendelea mbele na kufanya vizuri wakiwa pamoja kama kundi.


Akiongea kwa niaba ya wenzake, Gabu amesema kuwa P Unit ni kama familia na wanaheshimiana sana, Vitu vikubwa vinavyo wasimamisha ni 1]Mipango thabiti ambao wamejiwekea.

2] Wametambua tofauti kati ya kazi na urafiki. 

P Unit kwa sasa inabamba kwenye chati mbalimbali za muziki kwa ngoma yao ya You Guy ambayo wamemshirikisha King wa Rap, Collo ambaye naye pia anaiwakilisha vizuri Kenya.

 KUTOKA KWA SAMMISAGO

0 comments: